Episodes

  • Mezani na ASHA BARAKA #24
    Feb 14 2025

    AshaBaraka ni nani? Asha Baraka ni ASHA BARAKA. Unaweza kwenda mbali zaidi ukamuitaMama wa muziki wa dansi Tanzania na usiwe umemzidishia sifa. Asha Barakamwanamichezo kutoka Tabora Girls, Bima hadi kua kocha wa Netball(mpira wapete).

    Lakinileo tunakubaribisha kwenye safari yake kama mwanamke wa kwanza kumiliki bendiya muziki wa dansi Tanzania na mtanzania pekee ambae anaweza sema asilimiakubwa ya wanamuziki wanaofanya mziki wa dansi leo hii wamepita chini ya uongoziwake, iwe ni bendi au chuo cha kufundishia muziki.

    Jeni nani walikua wasanii wa kwanza kabisa Twanga? Banza Stone alikua mahirikiasi gani? Unafahamu Luiza Mbutu alifika fikaje Twanga? Kwanini Ally Chokianaitwa kinanda?

    Yotehaya ameyanyoosha kuweka rekodi sawa. Na ziada si haba. Karibu mezaniumsikilize The Ironylady, Mama, Bibi, Mkurugenzi na Chairman ila sisi tunamuitaNguzo kubwa ya mziki wa dansi Tanzania.

    Show More Show Less
    1 hr and 29 mins
  • Mezani na TAJI "MASTER T" LIUNDI #23
    Jan 3 2025

    Kama ulishawahi kuisikia ile story ya mtangazaji wa kwanza kucheza wimbo wa Bongo Fleva kwenye radio. Mtangazaji huyo, leo amepata nafasi ya kutubariki na historia yake. Jinsi alivyochangia muziki huu kuwa kimbilio la vijana wengi sana kama sehemu ya ajira yao.


    Jina lake kamili ni Taji George Liundi au MASTER T kama alivyobatizwa na Charles Hillary. Kuanzia alivyoanza kutangaza Redio One, moja ya vipindi vyake vya awali kabisa cha DJ Show, kabla ya kuwaachia mikoba wakina Mike Mhagama baada ya kuikacha Redio one na kwenda kufanya kazi kwenye media zingine.


    Karibu mezani umfahamu zaidi.

    Show More Show Less
    4 hrs and 13 mins
  • Mezani na LUCCI #22
    Nov 1 2024

    Marehemu CPWAA anatajwa kama mmoja wa wasanii wa kwanza kufanya muziki wa Crank (KING OF BONGO FLEVA CRANK) kupitia ngoma ya PWAA iliyotayarishwa na LUCCI chini ya Mawingu Studio. Hii inamaanisha kuwa Lucci ni mmoja wa waandaaji wa kwanza kwa muziki wa Bongo Fleva wenye mahadhi ya Crank. Mbali na kutayarisha muziki vilevile Lucci anasimama kama msanii baada ya kushiriki kwenye nyimbo kadhaa mfano Kaka na Dada aliyoshirikishwa na Jokate ambae kwasasa ni Katibu Mkuu wa UWT kupitia chama cha CCM.

    Show More Show Less
    1 hr and 54 mins
  • Mezani na DARK MASTER #21
    Sep 20 2024

    Bado kiwanda cha Bongo Fleva kinaendelea kukumbuka mchango mkubwa wa vijana walioiwakilisha Dodoma mwanzoni mwa mwaka 2001 kupitia ngoma zao kadhaa ambazo zinachezwa na kusikilizwa mpaka hivi sasa.


    Wanaitwa Chemba Squad, ambapo ndani yake majina kama Noorah aka Baba stylz, Dark Master, Albert Mangwea na Mez B wa area C yalitajwa kuunda kundi hilo.


    Ngoma kama Ice Cream, Ghetto langu na Kama Vipi zinatajwa kama ngoma bora za muda wote kutoka kwa wakali hao ambapo hivi sasa wamebaki wawili tu (Noorah yupo zake Shy Town na Dark Master akiwa Dar es salaam) huku bahati mbaya Ngwea na Mez B wakiwa ni marehemu (RIP).


    Leo tunakusogezea historia kamili na mengi usiyoyajua kuhusu Dark Master aka MwanaChemba.

    Show More Show Less
    1 hr and 30 mins
  • Mezani na FEROOZ #20
    Aug 2 2024

    Je Unamfahamu FERUZI MRISHO? Gwiji na moja wa waanzilishi na NUNDA mkuu wa DAZ NUNDAZ. Mwenyewe akitambulika zaidi kama Kamanda kabla Kamanda haijawa THE ANTHEM it is now. Leo tuko nae mezani akitusimulia safari yake yote ya mziki, toka anaandikiwa mashairi na dada yake Achane mpaka anatunga tungo matata kama Starehe, Kamanda, Nitafanya Nini, Jirushe, Elimu dunia N.K. Karibu Mezani.

    Show More Show Less
    1 hr and 36 mins
  • Mezani na MARLON LINJE #19
    Jul 18 2024

    Je, Unamfahamu producer ambaye, dare I say it, bila yeye labda kwaya au bendi yako maarufu usingeisikia kama ulivyoisikia? Producer ambaye amefanya zaidi ya 80% ya production ya mziki wote wa bendi na kwaya Tanzania kwa miaka 30. Marlon Linje, bonge la mshika dau, leo yupo nawe mezani, karibu.

    Show More Show Less
    2 hrs and 59 mins
  • Mezani na MANDOJO NA DOMOKAYA #18
    Nov 25 2022
    Usichofahamu ni majina yao halisi Joseph Francis Michael Ong'oso na Precious Juma Mkoma maarufu kama Man'Dojo na Domokaya. Wanamuziki mashuhuri sana wa kizazi cha jana na leo.  nani asiyepende kusikia sauti nzuri na za kuvutia zikisindikizwa na Guitar lao(wenyewe wanaliita Banjo)?  Nani asiyetambua uwezo wa miamba hawa wa muziki katika kuweka viitikio na vionjo makini katika nyimbo mbalimbali za Muziki wa Kibongo? Hawa ni marafiki waliogeuka ndugu, wenyewe wanadai wamepitia mpaka kuvaa nguo sare 😁 Meza Huru imekaa nao na kupata simulizi ya maisha yao ya muziki na amini kwamba, inavutia sana.  Jumuika nasi mezani kuwasililiza 😊, Karibu  #MezaniNaMandojoNaDomokaya  #MezaHuru
    Show More Show Less
    2 hrs and 31 mins
  • Mezani na KIBACHA Part II
    Nov 22 2022

    Sehemu ya pili ya maongezi yetu na KBC, ambaye wengi wanamfahamu kama Kibacha

    Huyu ni mojawapo wa mwamba muhimu wa Hip Hop ya Tanzania.

    Unaambiwa zama zake, Kipaza kilimuogopa kama ukoma, Rafiki wa mashairi na mchenguaji mashuhuri. Gwiji wa mtindo huru na Battle Emcee haswaaa. 

    Kibacha ni miongoni mwa waanzilishi wa Kundi kongwe na mahiri la KWANZA UNIT.

    Ametupa heshima kubwa ya kukaa nasi na kutupa historia ya muziki wake tangu miaka ya 80 mpaka hapa tulipo.

    Mwamba huyu hapa 😊

    #MezaniNaKBC 

    #MezaHuru 

    Show More Show Less
    1 hr and 41 mins