• TANAPA PODCAST EPISODE 16: MILA, DESTURI NA TAMADUNI KATIKA UHIFADHI WA MALIASILI.
    Nov 24 2025

    Episodi hii inaangazia njia za asili zilizotumika katika utunzaji wa maliasili kwa kufuata taratibu za kitamaduni, mila, desturi na makatazo mbalimbali yaliyosaidia kusimika mizizi imara na kuwa chimbuko la uhifadhi wa kisasa. Hekima za mababu zetu kama vile kuheshimu misitu, kutotumia rasilimali kupita kiasi, na kutambua uhusiano wa binadamu na mazingira vimekuwa dira muhimu inayoongoza mbinu za kisayansi za leo kwenye uhifadhi endelevu.


    Sikiliza simulizi hii ya kuvutia katika Epsodi ya 16.


    Mwongoza kipindi: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine Mbena.


    Mgeni I: Mzee Rashid Shabani

    Kitopeni.

    Mgeni II: Mzee Ramadhani Nyundo

    Usikose kila Jumatatu kupitia Platform za TANAPA Podcast.


    TANAPA PODCAST, HIFADHI ZETU, SAUTI YETU.

    Show More Show Less
    36 mins
  • TANAPA PODCAST EPISODE 15: UHIFADHI NI JUKUMU LA KILA MMOJA
    Nov 17 2025

    Episodi hii inakuletea uchambuzi wa kina kuhusu Uhifadhi kwa kuzingatia kuwa Uhifadhi wa wanyamapori ni zoezi la kujitolea kulinda na kuhifadhi maliasili kwa maslahi ya Taifa kwa kizazi hiki ma kijacho.


    Sikiliza Episodi ya 15 upate elimu kutoka kwa Mzee Ibrahimu Kasontola kutoka katika kijiji cha Lukoma wilayani Uvinza - Kigoma aliyejitolea kwa hali na mali kuhifadhi msitu katika eneo la makazi yake na kupelekea eneo hilo kuwa makazi ya kudumu ya Sokwemtu sanjari na kupanda migomba ambayo hutumika kama chakula pendwa cha wanyamapori hao ambao mara nyingi utawakuta katika makazi ya mzee huyo.


    Mwongoza Kipindi: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine Mbena.


    Wageni

    1.⁠ ⁠Ibrahim Kasontola (Mzee anayewahifadhi Sokwemtu hao).

    2.⁠ ⁠Mwatano Omary (Mke wa Mzee Ibrahim Kasontola).

    3.⁠ ⁠⁠Afisa Uhifadhi Mwandamizi - Lameck Matungwa Kaimu Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Milima Mahale

    Usikose kila Jumatatu kupitia Platform za TANAPA Podcast.

    TANAPA PODCAST, HIFADHI ZETU, SAUTI YETU.

    Show More Show Less
    1 hr and 3 mins
  • TANAPA PODCAST EPISODE 14: MILA, DESTURI NA TAMADUNI KATIKA UHIFADHI WA MALIASILI.
    Oct 27 2025

    Episodi hii inaangazia mila, desturi na tamaduni katika uhifadhi wa maliasili, hususan namna jamii ya Wangoni kutoka mkoani Ruvuma ilivyotumia majina na utamaduni wao kulinda Wanyamapori na Misitu tangu enzi za mababu zetu.

    Hadithi hii ya kuvutia inaonesha jinsi urithi wa jadi ulivyokuwa chachu ya kulinda rasilimali za Taifa ambazo leo hii zinachangia kwa kiasi kikubwa katika sekta ya uhifadhi na utalii.

    Sikiliza simulizi hii adhimu kutoka kwa Chifu Songea Mbano wa Kwanza, kupitia TANAPA Podcast – Episode ya 14.


    Mwongozaji: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine Mbena
    Mgeni: Samweli Vitus Mbano (Chifu Songea Mbano I)


    Usikose kila Jumatatu na Alhamisi kupitia majukwaa mbalimbali ya TANAPA Podcast

    Show More Show Less
    55 mins
  • TANAPA PODCAST EPISODE 13 - Mila na Tamaduni zilizohusisha mizimu katika kuhifadhi Maliasili
    Oct 20 2025

    Episodi hii inakuletea mazungumzo ya kina kuhusu mila, tamaduni na makatazo ya Kabila la Wagongwe lililopo mkoani Katavi na jinsi taratibu hizo zilivyochangia kulinda maliasili na vyanzo vya maji. Mathalani; ilikuwa hairuhusiwi kukata miti iliyokuwa katika vyanzo vya maji kutokaana na imani ya kuwepo kwa nyoka mkubwa wala kuua mnyamapori hadi upewe kibali na pepo au jini Katabi anayepatikana katika Hifadhi ya Taifa Katavi. Sikiliza simulizi hii ya kuvutia katika epsodi ya 13.Eneo: Hifadhi ya Taifa KataviMwongoza kipindi: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine Mbena Wageni:1.⁠ ⁠Moses Edward Tende ( Mtemi Sigulu) Chifu wa Kabila la Wagongwe.2.⁠ ⁠Lukas Moses Msaga - Mtoto wa Mtemi Sigulu anayefundishwa kurithi mikoba ya Mtemi Sigulu.⁠3.⁠ ⁠⁠Askari Uhifadhi Daraja la Pili - Kimori Shiwa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Ikolojia, Hifadhi ya Taifa Katavi. Endelea kutufuatilia kupitia Platifomu za TANAPA Podcast.TANAPA PODCAST, HIFADHI ZETU, SAUTI YETU.

    Show More Show Less
    55 mins
  • TANAPA PODCAST EPISODE 12 - Zoezi la Uhamishaji Tembo kutoka Misenyi kwenda Hifadhi ya Taifa Burigi - Chato.
    Oct 16 2025

    Episodi hii imeangazia zoezi endelevu la kuwahamisha tembo walowezi kutoka maeneo ya karibu na wananchi kwenda hifadhini na zoezi zima la kuwaswaga tembo waliotoka hifadhini kuvamia maeneo ya wananchi na kuwarudisha hifadhini.


    Sikiliza Episodi hii kwa taarifa hiyo na mengine mengi kupitia Epsode ya 12.


    Eneo: Misenyi - Bukoba.


    Host: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine Mbena


    Guests: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi Dkt. Fredrick Mofulu - Mkuu wa Hifadhi Ibanda - Kyerwa.

    Na

    Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi Charles Ngendo - Mkuu wa Hifadhi Rumanyika - Karagwe.


    Fuatilia kupitia Platform za TANAPA Podcast.

    Show More Show Less
    50 mins
  • TANAPA PODCAST EPISODE 11 - Nyumba ya Kumbukizi ya Mwl. Nyerere na Historia ya Taifa letu.
    Oct 13 2025

    Kuelekea Kumbukizi ya Kifo cha Hayati Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere Oktoba 14, TANAPA PODCAST tunakueletea uchambuzi kuhusu historia ya harakati za uhuru wa Tanganyika zilizoongozwa na Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere. Hapa utapata kujifunza mengi kuhusu harakati za Uhuru wa Tanganyika na Afrika kwa ujumla.


    Ikumbukwe historia hii imehifadhiwa katika Nyumba ya Kumbukizi ya Mwl. Nyerere iliyopo Magomeni Usalama jijini Dar es Salaam.

    Fuatilia uhondo huo katika Epsode ya 11.


    Eneo: Dar es salaam


    Host: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine Mbena

    Guest: Afisa Mhifadhi Mkuu Mariam Njaritha - Mkuu wa Kituo Nyumba Kumbukizi ya Mwl. Nyerere


    Usikose kila Jumatatu na Alhamisi kupitia Platform za TANAPA Podcast.

    TANAPA PODCAST, HIFADHI ZETU, SAUTI YETU.

    Show More Show Less
    42 mins
  • TANAPA PODCAST EPISODE 10 - MAANDALIZI YA TWENZETU KILELENI 2025 NA PROF. KAMUZORA
    Oct 9 2025

    Episodi hii inaangazia mazungumzo ya kina kuhusu zoezi la upandaji wa Mlima Kilimanjaro ambapo Profesa Kamuzora anaeleza uzoefu wake katika kupanda mlima kwa muda mrefu.


    Fahamu faida ya kushiriki kampeni ya “Twenzetu Kileleni katika kuadhimisha kumbukumbu ya uhuru wa Taifa letu, kuhamasisha utalii pamoja na utunzaji wa mazingira.


    Host: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine Mbena - Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano - TANAPA

    Guest: Prof. Faustin Kamuzora - Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi UTT AMIS.


    Show More Show Less
    45 mins
  • TANAPA PODCAST EPISODE 09 - YAFAHAMU MAENEO YA MALIKALE YALIYOKASIMISHWA TANAPA
    Oct 6 2025
    Episodi hii inaangazia maeneo ya Malikale yanayosimamiwa na TANAPA na faida zake. Maeneo hayo yamebeba historia za kale, biashara ya utumwa, utawala wa machifu, ukoloni na uhuru wa Taifa letu. Sikiiiza TANAPA PODCAST Epsode 09 upate elimu ya kina kuhusu historia ya Taifa letu, asili na umuhimu wa kutunza tamaduni zetu. Eneo: Dar es Salaam. Host: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine Mbena. Guest: Afisa Uhifadhi Mkuu Malikale, Neema Mbwana.
    Show More Show Less
    56 mins